Msanii anayefanya vizuri kwenye filamu na tamthilia Rayuuamesema kuwa kitendo cha yeye kunadamwa na skendo chafu za picha za ngono zimemfanya atofautiane na familia yake hasa wazazi, huku wakimtaka kuchukua hatua za haraka ili aweze kuachana na tabia hizo ambazo zinaweza kuichafulia jina familia.
Msanii huyo amekuwa akionekana kwenye picha za utupu ambazo zimekuwa zikimchafulia jina, alisema kuwa zimemfanya hadi kutoelewana na familia yake kwani wanahisi ni muhuni kitu ambacho si kweli.
“Familia yangu imechukia sana kutokana na picha zangu ambazo sijui watu wanazipata wapi, naonekana muhuni mbele ya wazazi wangu wakati siko hivyo, kuna watu wana nia ya kunifanya niwe mbaya mbele ya wazazi wangu na watu wanaonizunguka nashindwa kuelewa wananitafutia nini,” alisema.